Monday , 30th Mar , 2015

Kutoka kundi la Mapacha Watatu, Msanii wa Muziki Khaleed Chokoraa ameongea na eNewz na kueleza kurejea na mabadiliko makubwa katika muziki wao wa dansi.

Msanii wa muziki wa dansi nchini Khalid Chokoraa

Mabadiliko hayo makubwa ikiwepo kupunguza kutaja majina ya watu na vilevile urefu wa nyimbo kinyume na vile ilivyokuwa imezoeleka katika nyimbo nyingi za dansi hapa nchini.

Khaleed amesema kuwa, ujio huo mpya unakwenda sambamba na kuongeza ladha zaidi katika kazi zao, na albam yao mpya ambayo ipo katika hatua za mwisho sasa, ndiyo itakayoonesha mabadiliko hayo kwa kina.