Rayvanny katika FNL ya EATV
Rayvanny ameyasema hayo alipokuwa katika kipindi cha Friday Night Live cha EATV akiwa na Diamond Platnumz kuelezea mafanikio ya ngoma yao ya ‘Salome’ pamoja na namna wanavyofanya kazi katika kampuni ya WCB.
“Ninamshukuru Mungu, ninapata sapoti kubwa kutoka kwa mashabiki na ninaahidi kuendelea kufanya mambo mazuri zaidi na ninawaomba wazidi kuniunga mkono” Amesema Rayvanny.
Kuhusu ngoma ya Salome, Diamond amesema Rayvanny alipopewa ajaribu kuingiza sauti alionekana kuitendea haki zaidi, na ndiyo maana akaamua afanye naye ngoma hiyo badala ya mtu mwingine kutoka katika kampuni yao ya WCB.