
Nyanda na Naila wanaoliunda kundi moja la Brick and Lace amesema kuwa yeye na dada yake Naila wapo pamoja japokuwa Nail ameelekeza nguvu zake nyingi katika kazi za ubunifu wa ndani (interior design) wakati yeye Nyanda ameamua kufanya zaidi muziki.
Nyanda amesema kuwa hivi sasa wawili hao wamelamba mkataba na kampuni moja inayojishugulisha na usambazaji wa kazi za wasanii nchini Kenya itakayokuwa ikiwatangaza wasanii hao kupitia mitandaoni, na simu za mikononi barani Afrika.