Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wamiliki wachukuliwe hatua kumaliza ajali - Bashe

Thursday , 22nd Sep , 2016

Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini Hussein Bashe amesema ajali nyingi zinazotokea nchini zinagharimu maisha ya watu na mali lakini hazikomi kwa kuwa wamiliki hawawajibishwi ipasavyo na vyombo vyao vinabadilishwa majina kuendelea na kazi.

Hussein Bashe akiwa Kikaangoni

Bashe ametoa ushauri huo, alipokuwa KIKAANGONI ya ukurasa wa Facebook ya EATV, ambapo amesema kuwa serikali ni lazima ichukue hatua madhubuti kwa wamiliki wa mabasi ambayo yanasababisha ajali kwa kuwatoza faini pamoja na nyingine kuzifungia ili iwe fundisho kwa wengine.

“Mimi binafsi mwaka huu nimepoteza ndugu zangu wawili kwa ajali ya barabarani kutokana na uzembe wa hali ya juu wa madereva, na matukio haya yanapotokea mabasi yanashikwa na baada ya muda yanapakwa rangi nyingine na jina la kampuni linabadilishwa kazi inaendelea kwa namna hii hatuwezi kumaliza tatizo la ajali” Amesema Bashe.

Mbunge huyo amekwenda mbali zaidi na kutoa mfano wa vyombo vya habari ambapo , mwandishi akiandika habari yenye utata, mtu wa kwanza anayewajibishwa ni mmiliki wa chombo husika hivyo na kwa wenye kampuni za magari ya usafiri ikiwa hivyo itasaidia.

Aidha katika hatua nyingine Mbunge huyo akijibu swali kuhusu baadhi ya wabunge wa CCM kuitetea serikali kwa kila jambo, amesema si kweli wabunge wa CCM hutetea kila jambo linaloletwa na serikali bali kuna mambo huletwa na serikali na huyakataa kama yana utata.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya