Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mtoto wa miaka mitano kutolewa kizazi

Wednesday , 1st May , 2019

Mtoto wa miaka mitano mkazi wa Dodoma ambaye alipatwa na tatizo la kutokwa na damu sehemu za siri (hedhi) anatarajiwa kutolewa kizazi ili kuokoa uhai wake.

Kwa mujibu wa mama mzazi wa mtoto huyo, Bi. Loveness Samwa amesema kwamba mtoto wake huyo ambaye kwa sasa yuko hospitali ya Taifa ya Muhimbili akipatiwa matibabu, anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa kuondoa kizazi chake, ili kuzuia madhara zaidi yaliyotakana na kuvuja kwa damu.

Bi. Lovenes amesema kwamba baada ya kufika Muhimbili wakitokea Dodoma, binti yake akiwa amezidiwa, alipokelewa na kuanza kuhudumiwa, na mara baada ya vipimo ndipo akapewa majibu ambayo yatalazimu mtoto wake kutolewa kizazi.

"Tulifika hapa Muhimbili saa 4 asubuhi, madaktari walivyotuona wakaanza kumtibia kwanza mwanangu kwa sababu alikuwa bado hajapata fahamu, walimchukua na kuanza kumfanyia vipimo ambapo wakati nasubiria majibu walimtundikia maji wakamuwekea na Oxygen ambapo alikuja kuzinduka saa 11 jioni. Daktari aliniita tena kwa ajili ya kunipa majibu ambapo aliniambia kwamba kipindi mtoto wangu anapata siku zake, kuna damu ilienda kuganda kwenye kizazi, hivyo kusababisha kiharibike, kwa hiyo anatakiwa afanyiwe upasuaji ili kuondoa kizazi kwa lengo la kuokoa maisha yake", amesema Bi. Loveness.

Hata hivyo mama huyo amesema kwamba ili mtoto wake aweze kufanyiwa upasuaji anatakiwa alipie pesa shilingi laki nne, pesa ambayo amedai kuwa hana, na hata alizoanzia matibabu alichangiwa na watu.

HABARI ZAIDI

Mhe. George Simbachawene, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora

Waliohitimu mafunzo ya uongozi wafundwa uadilifu

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90