Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Nyangumi mjamzito afariki na kilo 22 za plastiki

Monday , 1st Apr , 2019

Mzoga wa nyangumi mjamzito ambao ulisombwa na maji hadi katika fukwe ya Sardinia nchini Italia, umekutwa na kilo 22 za plastiki tumboni pamoja na kichanga kilichokufa.

Nyangumi

Kwa mujibu wa Rais wa kundi moja la utunzaji mazingira la SeaMe nchini Italia, Luca Bittau, ameiambia CNN kuwa miongoni mwa vitu vilivyokutwa katika tumbo la nyangumi huyo ni mifuko ya uchafu, nyavu za kuvulia samaki, mabomba na mifuko ya sabuni za maji za kufulia nguo.

Nyangumi huyo mwenye urefu wa mita 8 na futi 26, alisombwa kutoka baharini hadi katika fukwe ya Sardinia, ambapo amesema kuwa chanzo cha kifo chake kitajulikana baada ya uchunguzi wa wataalamu wa wanyama nchini humo.

Naye Waziri wa mazingira wa Italia, Sergio Costa amesema kuwa serikali inalichukulia tatizo hilo kama changamoto kubwa katika utunzaji wa mazingira, akisisitiza kuwa nchi yake itakuwa ya kwanza kutekeleza sheria iliyopitishwa na bunge la Ulaya la kupiga marufuku kusambaa kwa vifungashio vya plastiki ili kulinda tishio la uhai wa viumbe wa majini.

Tukio lingine linalomhusu nyangumi

 

Licha ya tukio hilo, mwezi uliopita, nyangumi mwingine mdogo alikutwa amekufa nchini Ufilipino, akiwa na kilo 40 za plastiki tumboni.

Bonyeza hapa chini kutazama zaidi.

HABARI ZAIDI

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba