Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

 Magufuli aibuka na askari wachelewesha abiria

Monday , 10th Dec , 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amesema hafurahishwi na vitendo vya baadhi ya askari kukamata magari ya abiria na mizigo kisha kuyachelewesha kwa muda mrefu.

Rais Magufuli kushoto, pamoja na picha ya askari wa usalama barabarani wakiwa wamesimamisha basi la abiria.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam, kwenye Kikao cha kazi kati yake na Viongozi wa TRA pamoja na wakuu wa mikoa nchini, ambapo amekemea baadhi ya vitendo vinavyoharibu biashara za watu na kukwamisha ulipaji kodi.

''Askari anaweza kujisikia tu kusimamisha gari hata kwa zaidi ya saa 6 kisha akaliachia bila kujali kuwa hao ni wafanyabiashara na wanajisikia vibaya, kuharibiwa biashara zao wakapata hasara na mwisho wa siku wasilipe kodi. Mara nyingi hili linafanywa na jeshi la polisi'', amesema Rais.

Aidha Rais Magufuli ametoa agizo kwa mamlaka mbalimbali zinazohusika na kodi kuhakikisha zinaondoa vikwazo kwa walipa kodi pamoja na wawekezaji kutoka nje ya nchi.

''Pia nawataka TPA, TRA, Jeshi la polisi, Idara ya uhamiaji mjirekebishe kuna vitendo vingi vya kukwamisha wawekezaji na walipa kodi naomba mlifanyie kazi hilo nafahamu mengi kwahiyo mbadilike'', ameongeza.
 

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP