
Thomas Mashali
Akizungumza na East Africa Radio, Mashali amesema kwa sasa amejichimbia Bagamoyo mkoani Pwani, akifanya mazoezi makali kwa ajili ya pambano lolote litakalokuja mbele yake, akitarajia kuanza na Mmalawi katika mwezi wa Desemba mwaka huu.
Mashali, alishinda taji la dunia mkanda wa WBU, baada ya kumshinda kwa pointi bondia wa Iran, Sajad Mehrabi katika mwezi wa Mei mwaka huu, na inabidi autetee mkanda huo hivi karibuni.