Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

''Mkutano wa Yanga hauna mamlaka'' - TFF

Saturday , 17th Nov , 2018

Shirikisho la soka nchini (TFF) kupitia kwa Mwenyekiti wa kamati ya Uchaguzi, Malangwe Mchungahela imesema kwamba haimtambui Yussuf Manji kama  Mwenyekiti wa Yanga kwani katiba ya timu hiyo hairuhusu mkutano mkuu kumrejesha mwenyekiti aliyejiuzulu.

Mashabiki wa Yanga wakiwa makao makuu ya klabu hiyo,.

Hatua hiyo imekuja baada ya jana jioni wajumbe wa kamati  ya utendaji ya klabu ya Yanga kukutana na mwenyekiti huyo wa kamati ya uchaguzi wakiwa na hoja ya kukubali kufanya uchaguzi katika nafasi zingine isipokuwa nafasi ya Mwenyekiti.

"Sisi kama TFF hatumtambui Manji kama mwenyekiti  wa Yanga maana alishakutana na Waziri wa Michezo,  Dk Harrison Mwakyembe ili kuzungumzia suala la  kurudi Yanga na alimkatalia'', alisema Mchungahela.

Mchungahela alisisitiza kwa mujibu wa katiba ya  Yanga, Ibara ya 28 kanuni ya tatu (kifungu kidogo c), inasema mjumbe  atakoma kuwa mjumbe wa kamati ya utendaji iwapo  atashindwa kutekeleza majukumu ya mjumbe kutokana na kuumwa au sababu nyingine yoyote kwa  kipindi cha miezi 12 mfululizo.

Katiba hiyo ya marekebisho ya mwaka 2010, Ibara ya  14 inamruhusu mwanachama yoyote kujiuzulu na  kuwasilisha barua kwa katibu mkuu wa Yanga kwa barua ya rejesta. Mchungahela alisema kwa kuzingatia hilo hawamtambui Uenyekiti wa Manji.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya