Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba yapotea njia kwenye mashamba ya miwa

Wednesday , 18th Jan , 2017

Vinara wa ligi kuu Tanzania Bara imeanza kupoteza mwelekeo wa njia ya ubingwa wa ligi kuu Tanzania Bara baada ya leo kupotea njia kwenye mashamba ya miwa, na kulazimishwa suluhu na wakata miwa wa Mtibwa Sugar

Kiungo wa Mtibwa Ally Shomari akipambana na beki wa Simba Hamad Juma

Katika mchezo huo uliopigwa katika dimba la Jamhuri mjini Morogoro, Simba imeendelea kuonesha 'ubutu' katika safu yake ya ufungaji kwa kutengeneza nafasi nyingi lakini ikishindwa kuzitumia.

Kwa upande wa Mtibwa, waliingia uwanjani wakionesha kukamia mchezo huku wakiwa na mbinu ya kumaliza kwa sare kwa kuweka ukuta imara ulioongozwa na wakongwe Henry Joseph Shindika, Salim Mbonde, Vincent Barnabas, Issa Rashid 'Baba Ubaya' na kiungo Shaaban Nditi, hali iliyopelekea mchezo huo umalizike bila bao kwa upande wowote.

Akizungumzia mchezo huo, Nahodha wa Simba Jonas Mkude amekubali matokeo na kusema mpira una matokeo matatu, hivyo licha ya kutoyapenda, inabidi wayakubali kwa kuwa ndiyo matokeo ya mpira, na kuahidi kufanya vizuri zaidi katika michezo inayofuata.

Mshambuliaji wa Simba Shiza Kichuya baada ya kumfanyia madhambi Rashidi Mandawa  katika mchezo wao wa ligi kuu, Morogoro

Kwa upande wake Nahodha wa Mtibwa Sugar Shaaban Nditi ameshukuru kupata point moja katika mchezo huo, huku akitupia lawama ubovu wa uwanja na kusema wao hawakuzoea kufanya mazoezi katika uwanja huo, hivyo ubovu wa uwanja umechangia kuikosesha timu yake ushindi katika mchezo wa leo.

Matokeo haya yanaifanya Simba iendelee kubaki kileleni kwa kufikisha point 45, ikiwa ni point 2 mbele ya Yanga

Simba na Mtibwa ni timu ambazo wachezaji wake wengi wamewahi kuzichezea timu zote mbili yaani kuna wachezaji wa Simba waliotoka Mtibwa na kuna wachezaji wa Mtibwa waliotoka Simba, hivyo ni timu ambazo wachezaji wake wengi wanafahamiana

Mchezi ya Simba Vs Mtibwa katika mzunguko wa Kwanza ambapo Simba walishinda 2-0 katika uwanja wa Uhuru

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya