Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Tarehe ya Zana Coulibaly kucheza Simba yajulikana

Sunday , 9th Dec , 2018

Ni rasmi sasa, muda ambao mlinzi mpya wa klabu ya Simba, Zana Coulibaly ataanza kuonekana uwanjani umejulikana kwa mujibu wa kocha mkuu wa 'Wekundu hao wa Msimbazi, Patrick Aussems.

Mchezaji, Zana Coulibaly (kushoto), Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Crescentius Magori (katikati) na Kocha, Patrick Aussems (kulia).

Mlinzi huyo raia wa Burkina Faso alisajiliwa mapema mwezi uliopita akitokea klabu ya Asec Mimosas ya Ivory Coast kwa lengo la kuisaidia klabu hiyo katika michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na Klabu Bingwa barani Afrika baada ya kuumia kwa beki Shomari Kapombe.

Akizungumza juu ya muda wa mchezaji huyo kuanza kuichezea Simba, Aussems amesema kuwa hatoitumikia Simba katika michuano ya kimataifa mpaka pale watakapofanikiwa kutinga hatua ya makundi ya Klabu Bingwa barani Afrika kutokana na kuzuiwa kuingiza majina mapya katika hatua za awali.

"Siwezi kumtumia hivi sasa katika michuano ya kimataifa kutokana na sheria kutubana, lakini tukitinga hatua ya makundi nitaanza kumtumia," amesema Aussems.

"Huku kwenye ligi watu wataanza kumuona katika mzunguko wa pili kwa sababu hapo atakuwa fiti zaidi na naamini atakuwa msaada mkubwa kwenye timu na kuziba pengo la Kapombe," ameongeza.

Simba hivi sasa inajiandaa kwaajili ya mchezo wa hatua ya pili ya michuano ya Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Nkana FC ya Zambia, Disemba 15, mchezo ambao Simba itaanzia ugenini nchini humo.

Pia katika kuelekea mchezo huo, klabu ya Simba imetoa nafasi kwa mashabiki wake wanaotaka kwenda kuishangilia timu yao nchini Zambia, ambapo jumla ya nauli ya kwenda na kurudi ikiwa ni Sh 130,000. Msafara ukitarajiwa kuanza Alhamisi ya wiki ijayo na kufika nchini Zambia Ijumaa, siku moja kabla ya mchezo huo utakaopigwa Jumamosi.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja