Monday , 28th Mar , 2016

Mlinda Mlango wa zamani wa Yanga Peter Manyika amesema, wachezaji wanatakiwa kufuata yale mazuri yaliyokuwa yakifanywa na aliyekuwa mlinda mlango wa zamani wa Simba na Timu ya Taifa ya Uganda ‘The Cranes’, Raia wa Uganda Abel Dhaira aliyefariki jana.

Aliyekuwa Mlinda mlango wa Simba SC,Uganda na IBV Vestmanaeyjar ya Iceland, Marehemu Abel Dhaira

Manyika amesema, Dhaira alikuwa ni kipa aliyekuwa anastahili kucheza nje kutkana na kipaji chake na ndio maana hakukaa sana nchini mwake Uganda na Simba kwani timu zilikiona kipaji chake na kuweza kumchukua.

Dhaira amefariki hapo jana akiwa na umri wa miaka 28 na Januari mwaka huu ndiyo aligundulika kuwa na ugonjwa wa kansa ya utumbo.

Hadi mauti yanamkuta alikuwa bado ni kipa wa IBV Vestmanaeyjar ya Iceland.