
Vijana katika mazoezi ya Karate
Mwenyekiti wa TKA Sensei Willy Ringo, kwa niaba ya Kamati ya Utendaji ya Chama hicho amesema lengo ni kutaka kukutana na kuona umuhimu wa kuendeleza vipaji vya watoto wa shule za msingi katika mchezo wa Karate.
Mashindano hayo, yanatarajiwa kufanyika kati ya Oktoba 25-28, na kwa kuanzia, Ringo amesema gharama za kuleta vijana hao, zitakuwa za wazazi husika na shule zao, lakini baada ya mashindano kutakuwa na vyeti, na zawadi mbali mbali, kutoka Chama Cha Karate nchini.