
Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi Dr, Shabani Mwintanga amesema hayo jijini Tanga ikiwa ni sehemu ya mikakati iliyowekwa ya serikali katika kuhakikisha kuwa wagonjwa wa ebola wanadhibitiwa ili wasiweze kuingia nchini hasa katika mikoa ambayo inapakana na nchi jirani.
Dr. Mwintanga amewataka watendaji wa kiwanja cha ndege mkoani Tanga kuhakikisha wanadhibiti wageni kutoka nchi jirani ya Kenya na wanapohisi kupokea mgeni mwenye dalili hizo taarifa zitolewe kwa wataalam wa afya kisha apelekwe katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa tanga ''bombo''kwa ajili ya vipimo kabla ya kusafiri