Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba amla mtoto mbele ya mama yake

Tuesday , 6th Aug , 2019

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi Benjamin Kuzaga, ameeleza kutokea kwa tukio la mtoto mwenye umri wa miaka 6, aliyeuawa baada ya kuliwa na Simba, wakati akiwa amelala na mama yake katika Kijiji cha Sitalike wilayani Mpanda.

Tukio hilo limetokea mwishoni mwa wiki majira ya usiku, ambapo mtoto huyo akiwa amelala na mama yake  ndani ya nyumba ambayo haikuwa na mlango imara, walivamiwa na mnyama huyo.

"Walikuwa wanaishi nyumba ambayo haikuwa na mlango imara, huyu mtoto siku zote yuko na wazazi wake, siku ya tukio baba hakuwepo nyumbani. Ule udhaifu wa mlango ulichangia mnyama huyu kuingia ndani kirahisi," alisema Kamanda Kuzaga.

Inaelezwa mnyama huyo aliingia ndani na kumnyakua mtoto huyo na kisha kutoka naye nje, licha ya mama ake kupambania maisha na uhai wa mwanaye lakini juhudi zake hazikuzaa matunda baada ya mnyama huyo kutokomea gizani.

Baada ya polisi na wanakijiji kufika eneo la tukio, walikuta mtoto huyo tayari ameliwa na simba ambaye hawakuweza kumwona na kukuta mabaki ya kichwa na mifupa ya miguu pekee.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya