Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Namthamini yapiga mhuri kwa watu Tabora

Thursday , 15th Aug , 2019

Mkuu wa mkoa wa Tabora Mh. Aggrey Mwanri, ameipokea kampeni ya Namthamini ya East Africa Television na East Africa Radio, ambayo imefanikisha wasichana zaidi ya 1000 kubaki shuleni kwa mwaka mzima kwa kuwapatia taulo za kike.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akipokea taulo za kike kwaajili ya wanafunzi wa shule ya sekondari Ndono.

Akiongea leo Agosti 14, 2019 kwenye zoezi la ugawaji wa taulo za kike katika shule ya sekondari Ndono iliyopo wilayani Uyui, Mwanri amesema kitendao cha East Africa Television na East Africa Radio kupitia kampeni ya Namthamini, kupeleka pedi mkoani Tabora kimeweka alama ya kudumu.

''East Africa Television na East Africa Radio mmepiga mhuri katika mioyo ya watu wa Tabora, hatutakaa tusahau hili jambo mlilolifanya hapa'' - Mh Aggrey Mwanri Mkuu wa Mkoa wa Tabora.

Aidha Mkuu huyo wa mkoa ameiunga mkono kampeni ya Namthamini kwa kutoa kiasi cha shilingi Mil 1, kwaajili ya kuongeza taulo hizo katika shule za Ndono na Idete zote za wilayani Uyui.

Shule hizi mbili ni sehemu ya shule 4 zitakazopata pedi za kutosha wanafunzi kwa mwaka mzima mkoani Tabora. Huu ni mwendelezo wa zoezi la ugawaji wa Pedi hizo baada ya kuanza katika mikoa ya Arusha na Manyara.

Ikumbukwe kuwa kampeni ya Namthamini inaendelea kwa mwaka wa tatu sasa, na tayari imeshagusa maisha ya wanafunzi wa kike zaidi ya 5000 kote nchini.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda (Mwenye shati ya Bluu) akipata maelekezo wakati wa maonesho ya OSHA 2024 kwenye Viwanja vya General Tyres jijini Arusha.

RC ataka GGML iboreshe maisha ya wananchi Geita

Vijana Waliojiajiri Sekta ya Kilimo, Nigeria

Mishahara yaongezeka nchini Nigeria

Coaster iliyoparamia nyumba Bukoba

Tisa wanusurika kifo Kagera

Picha ya Fat Joe na Chris Brown

"Chris Brown anafaa kuwa 2Pac wa kisasa" - Fat Joe

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa