
Spika Ndugai ametoa kauli hiyo Bungeni jijini Dodoma leo, wakati wa kikao cha kwanza cha Mkutano wa 16, wa Bunge la 11, ambapo amesema katika Afrika Mashariki, Tanzania pekee ndiyo nchi ambayo Bunge lake bado linatumia karatasi.
Spika Ndugai amesema kuwa "sisi ndiyo Bunge pekee Afrika Mashariki ambao tunaendekeza Makaratasi mengi, wenzetu hawatumii, tunaanza na hii 'Order Paper' halafu tutaenda kidogo kidogo"
"Mpaka tufike hatua dawati la Mbunge liwe safi, naombeni mhakiki simu zenu na barua pepe, tunaanza kuwapatia nyaraka." ameongeza Spika Ndugai.
Leo Septemba 03, 2019 mkutano wa Bunge la 16 umeanza jijini Dodoma, ambapo Miraji Mtaturu aliapishwa kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, akirithi nafasi ya Tundu Lissu.