Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Baharia Kigwangalla abadili maamuzi

Tuesday , 10th Sep , 2019

Siku moja baada ya Mbunge wa Nzega Vijijini na Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla kuweka wazi kuwa amejiondoa kwenye chama cha Mabaharia, sasa ametangaza kurejea.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Kigwangalla ameeleza kuwa amepitia vizuri kanuni na miongozo ya chama hicho, na kugundua kuwa hazimpi nafasi ya kujiondoa.

''Ubaharia mtu hajiungi ukubwani, ni jambo la asili, unazaliwa nao! Huwezi kujitoa, wala baharia hazeeki. Baharia haachi wala hatolewi. Once a baharia always a baharia. Hivyo wazee wameniasa kwamba kwa ukongwe wangu, siwezi kujitoa maana sikujiunga, nabaki kuwa ‘baharia emeritus!’', ameandika.

Ikumbukwe kuwa Baharia ni Usemi ambao kwa sasa umekuwa ukitumika na watu mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii, ukimaanisha wanaume ambao wakisaidiana mara kwa mara, hasa kwenye masuala mbalimbali ikiwemo familia au kuunga mkono jambo wanaloamini wao.

Kwa mujibu wa Kamusi Sanifu, neno Baharia maana yake ni mtu anayefanya kazi kwenye chombo cha usafiri majini, hasa baharini kama vile boti, mashua, jahazi au meli. "Mwanamaji" hutumiwa mara nyingi kwa kutaja mabaharia wa kijeshi.

Tweet ya Kigwangalla imekuja muda mfupi baada ya Tinga namba moja kwa vijana East Africa Television, kurudi kibaharia kwenye King'amuzi cha Azam TV, kupitia Channel namba 118, na sasa unaweza kutazama burudani zote.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya