Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Droo ya nusu fainali yakamilika, michezo 3 kupigwa

Monday , 16th Sep , 2019

Droo ya hatua ya nusu fainali ya michuano ya Sprite Bball Kings 2019 imefanyika leo katika ofisi za EATV na EA Radio, ambapo vigogo wanne waliofuzu hatua hiyo wamepangwa katika mechi mbili.

Droo ya nusu fainali ya Sprite Bball Kings 2019

Timu zilizofuzu hatua ya nusu fainali ni KG Dallas, Flying Dribblers, Tamaduni na Mchenga Bball Stars ambapo kwenye hatua yenyewe ya nusu fainali, timu ya Flying Dribblers imepangwa na Mchenga Bball Stars huku KG Dallas ikipangwa na Tamaduni.

Kabla ya droo hiyo, baadhi ya wawakilishi wa timu za nusu fainali walitoa maoni yao, wa kwanza ni mwakilishi wa Tamaduni, Denis Babu ambaye alisema, "msimu huu tumejipanga zaidi ya mwaka jana, sisi tunataka hela tuu hatujali mtu yoyote hata kama droo isipochezeshwa, tangazeni tuu. Hawa Mchenga wataitwa mchanga tu".

Baada ya droo kupangwa, mwakilishi wa Flying Dribblers ambaye timu yake imepangwa na bingwa mtetezi Mchenga Bball Stars, amesema kuwa uzoefu umewasaidia sana kufika hapo na hawatofanya makosa kama msimu wa kwanza ambao walitolewa katika nusu fainali na mabingwa hao mara tatu mfululizo.

Michezo ya nusu fainali inatarajiwa kuwa mitatu ( best of three ), ambapo mchezo wa kwanza unatarajia kupigwa Jumamosi Septemba 21 katika Uwanja wa Ndani wa Taifa, mchezo wa pili utapigwa Jumatano Septemba 25. Eandapo washindi hawatapatikana katika 'best of two' mchezo wa tatu utapigwa Jumamosi Septemba 28.

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP