Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

'Asilimia 85 ya watu wana uono hafifu' - Dkt Frank

Wednesday , 9th Oct , 2019

Shirika la Afya Dunia (WHO), limeweka mpango mkakati wa kuhakikisha wanawake wanapewa kipaumbele cha kupatiwa matibabu ya afya ya macho, ambapo takwimu zinaonesha kuwa takribani asilimia 55 wana upungufu wa kati wa kuona.

Vipimo vya macho

Hayo yamebainishwa leo Oktoba 9, 2019 na Rais wa Chama cha Madaktari wa Macho nchini Dkt Frank Sandi, ikiwa ni katika kuelekea wiki ya Afya ya macho Duniani, inayoadhimishwa kila Alhamisi ya pili ya mwezi Oktoba, ambayo kwa mwaka huu imeangukia Oktoba 10, 2019.

''Takribani watu bilioni 1.3, wanakadiriwa kuwa na upungufu wa kuona na asilimia 85 wanaishi katika nchi zenye kipato cha chini, ikiwemo nchi ya Tanzania'' amesema Dkt Sandi.

Kwa upande wake Makamu Rais wa Chama hicho Dkt Cyprian Ntomoka, amesema kuwa watu wengi wamekuwa wakitafuta huduma ya macho yao, wakiwa wamechelewa hali inayopelekea kuwa na idadi kubwa ya watu wenye matatizo hayo.

''Watu wengi wanaishi maisha magumu, unakuja unamuuliza amekujaje anakujibu amekuja kwa kuendesha gari, wakati hana uwezo wa kuona na ukiangalia Sheria ya nchi hairuhusu mtu kuendesha gari akiwa na hali hiyo ni muhimu mtu akapima macho mapema ili aweze kutibiwa'' amesema Dkt Ntomoka.
 

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP