Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Vijana waaswa kuacha ngono maana sio Mlo kamili

Sunday , 1st Dec , 2019

Mwenyekiti wa Baraza la watu wanaoishi na Ukimwi hapa nchini (NACOPHA), Leticia Kapela, amewataka vijana kujiepusha na ngono isiyo salama, sanjari na kuwaonya vijana wanaopenda kujihusisha kimapenzi na watu wazima hii ni kutokana na kuwepo kwa ongezeko kubwa la vijana wanaoishi na ugonjwa

Hayo ameyabainisha leo Desemba 1, 2019, Jijini Mwanza, wakati wa kilele cha Maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani na kuwataka wanaume watu wazima, wanaowarubuni mabinti kuingia nao katika mahusiano ya kimapenzi waache tabia hiyo.

"Vijana tutumie kinga sababu nikisema watu muache hamuelewi kabisa, acheni ngono, kwani lazima ufanye? mmeambiwa hicho ni chakula ambacho ukiacha kukila utapata Utapiamlo?, lakini pia kuna tabia ya vijana wadogo kuomba kulelewa na wanawake watu wazima kama mimi, unakuta kijana anakufuata anaomba umlee unamuuliza kwani wewe huna wazazi?" amesema Leticia.

Aidha Mwenyekiti huyo ametoa rai kwa jamii nzima, kuacha kutumia neno waathirika pindi wanapowaita watu wenye Virusi vya Ukimwi.

"Sisi watu tunaoishi na Virusi vya Ukimwi, tumekuwa tukikwaza na neno kuitwa waathirika, neno waathirika lina unyanyapaa ndani yake, ambao ni tishio kuliko Virusi vya Ukimwi vyenyewe, tungependa tuitwe watu wanaoishi na Virusi vya Ukimwi, kwasababu hakuna aliyetuma maombi ya kuomba ugonjwa huu", amesema Leticia.

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya