Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Naibu waziri Ndumbaro aimaliza Yanga dhidi Simba

Saturday , 4th Jan , 2020

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mh Damas Ndumbaro, ambaye ni shabiki mkubwa wa klabu ya soka ya Simba na amewahi kuiongoza kwa nyakati tofauti, amesema timu yake hiyo ina nafasi kubwa ya kushinda kwenye mchezo wa leo.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mh Damas Ndumbaro

Akiongea na EATV, Ndumbaro amesema Simba kwasasa ina kikosi kizuri na kinaweza kucheza na timu yoyote na pia ipo katika hali nzuri kiuchumi hivyo ina kila sababu ya kushinda pambano la watani wa jadi.

'Unajua Simba wana viwanja vyao vya mazoezi hivi sasa lakini Yanga bado wanahangaika mpira umewashinda wanahangaika na vifusi pale kwao na mafuriko haya unaweza kufuga hata kambale pale, kwahiyo tarehe 4 ni msiba mkubwa', amesema.

Mchezo huo ni wa kwanza kwa watani wa jadi msimu huu, ambapo utapigwa leo kwenye uwanja wa Taifa Dar es salaam kuanzia saa 11:00 jioni.

Simba kwasasa wanaongoza ligi wakiwa na pointi 34 kwenye mechi 13 huku tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa ni 24. Yanga wapo nafasi ya 3 wakiwa na pointi 24 kwenye mechi 11 na wastani wa magoli ya kufunga na kufungwa ni 6.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya