Monday , 13th Jan , 2020

Kampuni ya kiteknolojia ya Microsoft imetoa tahahadhari kwa watumiaji wa mfumo endeshi wa kompyuta wa Windows 7 kuwa ifikapo Januari 14 haitatoa msaada kwenye vifaa vyao.

Mfumo endeshi wa Windows 7

Hatua hiyo imekuja ikiwa ni katika mchakato wake wa kuachana na teknolojia hiyo ambayo inasema imepitwa na wakati.

Mfumo endeshi wa Windows 7 ulizinduliwa na kampuni hiyo kwa mara ya kwanza Oktoba 22, 2009, ambapo imesema nia yake ni kuachana nayo na kujikita zaidi katika teknolojia mpya za sasa na zile ambazo watazivumbua.

Baada ya Januari 14, 2020, msaada wa ku'update software, ku'update mfumo wenyewe havitopatikana kwenye kompyuta zinazotumia mfumo huo, ambapo wanashauriwa kuhamia kwenye mfumo endeshi wa Windows 10 ili kuepukana na usumbufu wowote utakaotokea.