Mbwana Samatta na Waziri Mwakyembe
Waziri Mwakyembe ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na EATV na EA Radio Digital ili kupata kauli ya Serikali kuhusiana na hatua aliyofikia Mbwana Samatta.
Mwakyembe amesema kuwa "hakika kama Serikali tumefurahi kama walivyofurahi Watanzania wote, tunampongeza sana Samatta kwa juhudi zake najua hakubahatisha, ila kwa nidhamu ya hali ya juu, na hiki ndiyo kinawakwamisha vijana wengi wa Kitanzania mtu akikupa safari mbili unajiona umemaliza." - Waziri Mwakyembe
"Wanaotaka @Samagoal77_ ajengewe sanamu, wasikimbilie masuala ya sanamu, tumuombee afanye vizuri kwanza, hata tukijenga sanamu lakini asipofanya vizuri Aston Villa haitaleta maana, alipofika Samatta sio kilele cha mafanikio tunataka awe Messi wa Dunia nyingine" - Waziri Mwakyembe pic.twitter.com/4QPZ6zTrzS
— East Africa Radio (@earadiofm) January 21, 2020
Tazama video kamili hapo chini