Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manara ajibu kuhusu kuondoka 'Karantini'

Friday , 27th Mar , 2020

Afisa Habari wa Simba, Haji Manara amezungumzia kuhusu kitendo chake cha kuhudhuria mazishi kabla ya siku 14 za kujitenga kutokana na tishio la virusi vya Corona.

Haji Manara

Jana Machi 26, 2020, Manara alihudhuria mazishi ya aliyekuwa Msemaji wa klabu hiyo,  Asha Haji aliyefariki Machi 25 katika hospitali ya Hindu Mandal Jijini Dar es Salaam, ambapo alitokea katika Karantini yake ambayo aliiandaa mwenyewe kwa siku 14 baada ya kurejea nchini akitokea katika ziara yake barani Ulaya.

Katika ukurasa wake wa Instagram, Manara amesema kuwa yeye hana maambukizi ya virusi vya Corona baada ya kupima mara mbili hapa nchini na aliamua kujiweka Karantini kwa hiyari yake, hivyo hajakatazwa kuhudhuria shughuli yoyote.

"Wapo watu wananilaumu eti kwanini nimeenda msibani wakati nipo katika Karantini?. Niwafahamishe ni mimi binafsi kwa hiyari yangu niliamua kukaa Karantini baada ya kutoka safari bila kushurutishwa na yoyote!", amesema Manara.

"Agizo la Mh Rais la kuwataka wote wanaorejea kutoka nje kukaa Karantini kwa siku 14, limetolewa mimi nikiwa tayari nimesharejea, nilipimwa mara mbili hapa nchini na kubainika nipo salama lakini nikasema ngoja nikae mwenyewe kidogo kujisikilizia. Sasa kwa msiba wa dada yangu na kwa kuwa nipo salama baada ya vipimo vya kitabibu kuonyesha hivyo, sikuweza kukaa ndani tena", ameongeza.

Manara pia amesema kuwa watu wanaomlaumu ni wale ambao wanamuombea mabaya ili asifanikiwe.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Makamba

Ziara ya Rais Samia Korea kuanza rasmi Mei 31 2024

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20