Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Wagonjwa wa Corona walitaka kutoroka" - DC Ilala

Thursday , 23rd Apr , 2020

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema, amesema kuwa bado hajapata taarifa za waathirika wa Virusi vya Corona, waliopo katika kituo maalum katika Hospitali ya Amana, kama wametoroka na kurejea makwao ila anachojua walikuwa wanatishia kuondoka kwa madai ya kuwa hali zao kiafya ni nzuri.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema.

Mjema ameyabainisha hayo leo Aprili 23,2020, wakati akizungumza na ITV, kufuatia taarifa mbalimbali zilizokuwa zikisambaa kwenye mitandao ya kijamii zikieleza kuwa, baadhi ya wagonjwa katika hospitali hiyo wameleta vurugu na wengine kutoroka.

"Bado hatuna taarifa ya wagonjwa katika Hospitali ya Amana waliotoroka na kupanda daladala kurejea makwao, ngoja tuifuatilie ila tunachojua ni kwamba walikuwa wanasema wanataka kurudi nyumbani, kifupi walikuwa wanatishia tu" DC Ilala, Sophia Mjema.

Aidha DC Mjema ameongeza kuwa "Kulikuwa na wagonjwa ambao walikuwa wamefika pale na kusema kuwa wao hawaumwi sana kwahiyo walikuwa wanataka waruhusiwe na unajua ukifika pale, ukiwa mshukiwa lazima ukae kidogo hospitali uangaliwe wakuone upo vizuri ndiyo uruhusiwe".

EATV&EA Radio Digital, ilimtafuta Mkuu huyo wa Wilaya kwa ajili ya kupanda undani wa taarifa hizo, ambapo alidai kuwa yupo kwenye kikao na akitoka basi atatupigia simu na kutueleza ni kipi kilichojiri na hatua zipi ambazo zimekwishachukuliwa hadi sasa.
 

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP