Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Muimbaji Nyota azungumzia kifo cha Mzee Njenje

Sunday , 24th May , 2020

Muimbaji wa Bendi ya Kilimanjaro, Nyota Waziri, amezungumzia kifo cha Mkongwe wa Bendi hiyo Mabrouk Omar maarufu kama Mzee Njenje, na kusema kuwa alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya muda mrefu yaliyosababishwa na uzee.

Muimbaji wa Bendi ya Kilimanjaro, Nyota Waziri na kulia ni Mzee Njenje.

Hayo ameyabainisha leo Mei 24, 2020, wakati akizungumza na EATV&EA Radio Digital, ambapo pia tulizungumza na ndugu wa karibu wa Mzee Njenje na kwa pamoja walikuwa na haya ya kusema.

"Ni kweli amefariki leo Alfajiri na alikuwa anaumwa kwa muda mrefu, na juzi hapa alianza kuumwa tena, mazishi ni leo anazikwa Makaburi ya Kisutu" amesema Nyota Waziri.

Kwa upande wake ndugu wa karibu wa Mzee Njenje aliyejitambulisha kwa jina la Naima George amesema kuwa, "Alikuwa anaumwa na hali imebadilika tangu juzi, tulimpeleka Hospitali akapata huduma ya kwanza, Daktari akashauri apumzishwe kwa siku tatu, bahati mbaya leo Mungu kampenda zaidi, alipa stroke na ilimjia kama mara mbili hivi, lakini pia alikuwa anasumbuliwa na macho, figo na presha pia, ana watoto wawili na mke mmoja".

Mzee Njenje amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 73 na mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na mara baada ya kuswaliwa utapelekwa moja kwa moja katika makaburi ya Kisutu kwa ajili ya mazishi hii leo.

Ikumbukwe kuwa Mzee Njenje, alitamba na nyimbo kama, Kinyaunyau, Kachiri, Ndembere pamoja na Boko.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava