Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

"Nitachaguliwa na Zitto ataachwa" -Abdul Nondo

Sunday , 5th Jul , 2020

Mwenyekiti wa Ngome ya vijana wa ACT Wazalendo Abdul Nondo amesema kuwa hakuona haja ya yeye kumshirikisha Zitto Kabwe kama anataka kutia nia ya kugombea Ubunge katika Jimbo la Kigoma Mjini  kwa kuwa chama hicho kinazingatia demokrasia na kwamba hakina Papa bali wanachama wote ni sawa.

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa ACT Wazalendo, Abdul Nondo.

Abdul Nondo ametoa kauli hiyo leo Julai 5, 2020, wakati akizungumza na EATV&EA Radio Digital, na kusema kuwa endapo vikao vya chama chake vitampa ridhaa ya kupeperusha bendera ya kugombea Ubunge, basi atahakikisha anatekeleza na kuyaendeleza yale yote aliyoyaanzisha Mbunge mstaafu wa jimbo hilo Zitto Kabwe.

"Inawezekana mimi nikachaguliwa na Zitto akaachwa kwa sababu chama chetu kinaongozwa kwa mfumo wa demokrasia ya wazi, kwahiyo wajumbe wanaweza wakaamua kwa sababu chama chetu hakina Papa, kinasema wote ni sawa haijalishi wewe ni nani, Wajumbe wanaweza wakaamua kunichagua mimi, au wakaamua kumchagua Zitto halafu mimi wakaniambia nisubiri" amesema Nondo.

Leo Julai 5, 2020, Abdul Nondo ametangaza nia ya kugombea nafasi ya Ubunge katika jimbo la Kigoma Mjini, ambalo kabla ya Bunge kuvunjwa, lilikuwa likiongozwa na kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe.

Tazama Video hapa chini.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya