Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Chanzo kifo cha Rais Mkapa chatajwa

Sunday , 26th Jul , 2020

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mwanafamilia wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Benjamin William Mkapa, William Erio, imeeleza kuwa siku ya Jumatano Rais Mkapa alilazwa Hospitali baada ya kugundulika kuwa na Malaria, lakini baadaye aliaga Dunia kutokana na mshituko wa Moyo.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Marehemu Benjamin William Mkapa.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Julai 26, 2020, wakati wa Ibada ya kuaga mwili wa Rais Mstaafu katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam na kuwataka Watanzania kuendelea kumuenzi Rais Mkapa na kuachana na maneno ya mitandaoni ambayo yameanza kutoa taarifa za kifo chake ambazo siyo sahihi.

"Mzee wetu alikuwa hajisikii vizuri akaenda Hospitali na baada ya kuchukuliwa vipimo akakutwa na Malaria, akaanza matibabu na alilazwa siku ya Jumatano, mimi binafsi nilikuwa naye mpaka saa 2:00 usiku, baada ya kusikiliza taarifa ya habari aliinuka na akainamisha kichwa na mpaka walipokuja kumpima akawa amefariki, sababu ya kifo alipata mshituko wa Moyo" amesema William.

Aidha Erio ameeleza sababu iliyopelekea kueleza chanzo cha kifo chake, "Nilidhani ni vizuri tuliseme hivi kwa sababu kumeanza kuwa na maneno maneno kwenye mitandao, niwaombe na kuwasihi Watanzania wenzangu tumuenzi Mzee wetu aliyetangulia mbele ya haki kwa kuheshimu ukweli huo, kwamba hicho ndicho kilichosababisha kifo chake".

 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya