Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mchujo CCM, wajumbe kazini leo

Thursday , 30th Jul , 2020

Mchakato wa mchujo kwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walioomba kugombea Udiwani, unaanza leo kwa vikao vya chama hicho vya Kata kuwajadili wagombea. 

Bendera za CCM

Kwa upande wa wagombea Ubunge na uwakilishi kwa Zanzibar, vikao vya majimbo pia vinaanza leo, huku vikao vya Wilaya kwa upande wa Tanzania Bara, vinatarajiwa kuanza keshokutwa hadi Agosti 2, mwaka huu.

Tayari CCM imekamilisha mchakato wa kura za maoni kwa ngazi ya Ubunge, Udiwani na uwakilishi, ulioanza tangu Julai 14 na kukamilika Julai 17, mwaka huu, kwa mara ya kwanza katika historia ya CCM, kulikuwa na idadi kubwa ya wanachama waliojitokeza kuchukua fomu, kuomba kuteuliwa kugombea nafasi hizo, kwa ngazi ya Ubunge pekee, jimbo moja idadi ya chini ya wanachama waliojitokeza ilikuwa si chini ya watu 30.

Dar es Salaam kuna Wilaya tano na majimbo 10, ambapo Wilaya ya Ubungo ina majimbo ya Ubungo na Kibamba, Wilaya ya Kinondoni ina majimbo ya Kinondoni na Kawe na wilaya ya Temeke ina majimbo ya Mbagala na Temeke.

Aidha, wilaya ya Ilala ina majimbo ya Ilala, Segerea na Ukonga na Wilaya ya Kigamboni ina jimbo moja la Kigamboni. 

Baada ya vikao vya Kata kujadili wagombea wa udiwani, vitatoa mapendekezo kwa kamati za siasa za wilaya, ambazo zitatoa mapendekezo kwa Halmashauri Kuu za Mikoa ambazo zitajadili wagombea na kuteua wagombea wa udiwani mmoja katika kila kata mkoani humo. 

Kwa upande wa Ubunge, baada ya vikao vya wilaya kupendekeza majina ya wagombea watakaokiwakilisha chama hicho kwenye Uchaguzi Mkuu Oktoba 28, mwaka huu, maoni ya vikao hivyo yatawasilishwa kwa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM. 

Kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt John Magufuli itateua jina moja la mwana CCM ,atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi wa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya