Sunday , 9th Aug , 2020

Rais Magufuli amemteua Ngw'ilabuzu Ludigija kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala akichukua nafasi ya Mussa Chogelo ambaye amepangiwa kazi nyingine kwenye ofisi ya Rais, kabla ya uteuzi huo Ludigija alikuwa ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.

Uteuzi huo umefanyika hii leo Agosti 9, 2020, na tarifa hiyo kutolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, ambapo pia Rais Magufuli amemhamisha kituo cha kazi Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mpimbwe mkoani Katavi Erasto Kiwale, ambaye atakwenda kuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kigamboni.

Aidha Rais Magufuli amemteua Catherine Mashalla kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mpimbwe, ambapo kabla ya nafasi hiyo alikuwa ni Afisa Elimu wa Manispaa ya Kigamboni, ambapo uteuzi pamoja na uhamisho wa viongozi hao unaanza leo.