
Msanii wa BongoFleva Aslay Isihaka
Kupitia post yake aliyoweka kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram msanii huyo ameeleza kuwa "Inasikitisha na kushangaza sana unawezaje kumzushia mwanadamu mwenzako kifo na mabaya mengi, wanaofanya hivi ni Watanzania wa kawaida kama sisi ambao tulitamani watupe habari na burudani na wao wapate riziki, lakini wako bize kutupotosha na hata kuharibu majina yetu"
"Nawaomba sana TCRA wasiache kuzichukulia hatua online Tv makanjanja wengine wanaopotosha umma, tuna imani nanyi TCRA na Jeshi la Polisi na mamlaka nyingine, watu kama hawa wakiachwa, wanachafua taswira nzuri ya vyombo vingine vinavyofanya kazi kwa weledi, naheshimu sana waandishi wote bila kujali ukubwa wa vyombo vyao, lakini hawa makanjanja wachukuliwe hatua na kutokomezwa kabisa" ameongeza
EATV & EA Radio Digital imejaribu kumtafuta msanii huyo ili kutolea maelezo zaidi lakini imeshindikana kumpata hewani kwa sababu alikuwa hapatikani.