Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Daktari azungumza suala la kujamba na kutoa harufu

Thursday , 27th Aug , 2020

Daktari kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS), Dkt William Mawala, amesema kuwa mtu anayepitisha gesi yenye harufu kali inaweza kuwa ni kiashiria cha tatizo mwilini ikiwemo matatizo kwenye mfumo wa chakula.

Kujamba

Akizungumza na SupaBreakfast ya East Africa Radio hii leo Agosti 27, 2020, Dkt Mawala amesema kuwa binadamu hutoa gesi mara 5 mpaka mara 15 kwa siku, ikiwa ni jambo la kawaida kwa mwili kufanya hivyo kutokana na kazi za mwili.

"Kupitisha gesi kwa wingi kwenye njia ya haja kubwa, inaweza kuwa ni ya kimyakimya na isiyo na harufu au ya sauti na inaweza kuwa ni mchakato wa kawaida au shida kwenye mfumo wa chakula, sababu inayosababisha ni ulaji wa vyakula vyenye nyuzi lishe nyingi kwani huchelewa kumeng'enywa, vyenye madini ya sulphur, mayai, nyama, zingine ni athari za madawa mbalimbali na kuwa na tatizo la kutokupata choo kwa muda mrefu", amesema Dkt Mawala

Amesisitiza watu kuacha kutafuna 'bigjii', kula harakaharaka na kuacha kunywa vinywaji vyenye gesi ili kuepukana na tatizo la tumbo kujaa gesi.
 

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya