Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Watoa huduma mtandaoni wafundwa uchaguzi mkuu

Tuesday , 15th Sep , 2020

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imewataka watoa huduma ya habari mitandaoni kuwa makini na kuepuka joto la uchaguzi ambalo watu wengi hushindwa kustahimili hasa katika kipindi hiki cha kampeni za urais, ubunge na udiwani katika uchaguzi mkuu.

Mkurugenzi wa Uchaguzi Dk. Charles Mahera

Mapema hii leo Mkurugenzi wa Uchaguzi Dk. Charles Mahera wakati akizindua kikao kati ya tume ya uchaguzi na watoa huduma ya habari mitandaoni amewataka pia kutumia kalamu zao kulinda amani iliyopo huku akionya kuwa tume inawauwezo wa kuwachukulia hatua wadau wa uchaguzi wasiozingatia mioangozo ya maadili iliyosainiwa.

Aidha, vijana wametakiwa kujiajiri kwenye sekta hiyo huku wakizingatia kuheshimu taratibu za usajili zilizowekwa na mamlaka mbalimbali ikiwemo Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) huku wakikumbushwa jinsi NEC inavyoendelea kuweka uwanja sawa kwa washiriki wote wa uchaguzi mkuu ujao. Ambapo baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamesema yamekuja katika wakati mzuri.

Kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi imesema lengo la kikao hicho kwa watoa huduma ya habari mitandaoni ni kuongeza kukumbushana kuwa kuna maisha mengine baada ya uchaguzi mkuu hivyo ni muhimu kutumia lugha yenye staha kipindi chote cha uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 28,2020.

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP