Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Alcantara kutua Liverpool kwa dau la bilioni 74

Thursday , 17th Sep , 2020

Klabu ya Liverpool inakaribia kukamilisha usajili wa kiungo Thiago Alcantara  kutoka Bayern Munich ya Ujerumani kwa ada ya uhamisho ya fedha za Uingereza pauni milion 25 ambayo ni zaidi ya bilioni 74 kwa pesa za kitanzania.

Alcantara ameshinda mataji 16 katika misumu saba akaiwa na kikosi cha Bayern Munich

Kiungo huyo raia wa Hispania amekuwa akihusishwa kujiunga na Liverpool toka mwezi julai baada ya kuweka wazi kuwa hata saini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia the Bavarians pindi mkataba wake utakapo malizika mwishoni mwa msimu huu.

Hivyo Bayern wamefikia uamuzi wa kumuuza katika dirisha hili la kiangazi kwani endapo kama wangemuacha aondoke mwishoni mwa msimu huu wasingepata chochote angeondoka akiwa mchezaji huru.

Katika uthibitisho kuwa kiungo huyo anaondoka asubuhi ya Leo Mwenyekiti wa Bayern Minich Karl-Heinz Rummenigge amethibitisha kuwa klabu yao imefikia makubaliano na Liverpool na Thiago anaondoka.
'FC Bayern imefikia makubaliano na Liverpool, Thiago anaondoka' amesema Karl-Heinz Rummenigge

Liverpool italipa kwanza ada ya uhamisho ya pauni milion 25 ambayo ni zaidi ya bilion 74 kwa pesa za kitanzana na wataongeza pauni milion 5 ambayo ni zaidi ya bilion 14 kwa pesa za kitanzania endapo kama kikosi cha Liverpool kitashinda ubingwa wa klabu bingwa ulaya au ubingwa wa ligi kuu England EPL.

Alcantara mwenye umri wa miaka 29 ameshafanya mazungumzo binafsi na liverpool atasaini mkataba wa miaka minne wa kuitumikia Liverpool na atavaa jezi namba sita, kilichobaki ni kufanya vipimo vya afya kabla ya kutangwa kuwa mchezaji rasmi wa Liverpool.

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali