
Mgombea urais kupitia CCM Dkt John Pombe Magufuli.
Akizungumza hii leo Oktoba 14, 2020, wakati akihitimisha kampeni zake katika mkoa wa Dar es salaam viwanja vya Tanganyika packers amesema kwa mapendekezo yaliyotolewa na viongozi wa CCM, Joseph Gwajima anafaa kuwa mbunge wa Kawe.
''Ninataka kawe ibadilike,nataka kawe tutengeneze ajira za vijana,kwanini Kawe hakuna viwanda vingi wakati Pwani kuna viwanda vya kutosha mpaka Mkuranga vimejengwa'', amesema Dkt. John Magufuli
Pia Dkt Magufuli ameongelea haya, ''Tumepanga kujenga viwanda vya kuchakata samaki, kwanini visijengwe Kawe, vijana wetu wakapata ajira? tunahitaji mtu mwenye mipango, tunahitaji mtu mwenye 'connection' na serikali''.
Joseph Gwajima ni mgombea wa Kawe kupitia CCM akichuana kwa ukaribu na mgombea wa CHADEMA Halima Mdee, kupitia jimbo hilo