Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu
Akizungumza na wananchi waliodhuria mkutano huo leo, Oktoba 18, Mama Samia amesema kuwa yupo kwa ajili yakumuwakilisha Rais Magufuli, ambaye amefanya kazi kubwa sana ya kuzunguka nchi nzima na kuongea na wananchi.
“Niko hapa kwa niaba ya Mhe.Rais Dkt. John Pombe Magufuli, ambaye alitaka sana kuwa nanyi leo lakini kama mnavyojua tumefanya kazi kubwa yakuzunguka nchi tumeongea sana ameongea sana Dar es salaam, kwa kweli mpaka ananipigia simu nikamwambia Mheshimiwa pumzika mimi naenda" alisema Mama Samia
“Najua hivyo yuko ofisini anaendelea na kazi kwa hiyo nipo hapa kwa ajili yake na nitasema yale ambayo angekuwepo angesema na nitapokea yale ambayo mmeniambia niyabebe nimpelekee bila kuongeza wala kupunguza" aliongeza Mama Samia
Leo sekta binafsi imefanya makutano kwa ajili ya kumpongeza Rais Dkt.John Magufuli kwa mafinikio yaliyopatikana chini ya uongozi wake kwa muda wa miaka mitano huku Mama Samia Suluhu, akiwa mgeni rasmi akimuwakilisha Rais Magufuli.