Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Familia yasusa kuzika, yadai polisi wanahusika

Tuesday , 15th Dec , 2020

Familia ya kijana Masudi Said (24), iliyopo katika Kijiji cha Irungu wilayani Magu mkoani Mwanza, imegoma kuzika mwili wa marehemu kwa takribani siku nane kufuatia kuwepo kwa utata wa kifo cha kijana huyo.

Saidi Haruna ni baba mzazi wa Masudi Saidi.

Familia hiyo inadai kuwa siku ya Desemba 3, 2020, majira ya usiku kijana wao akiwa amelala aligongewa mlango na Mwenyekiti wa Kijiji hicho anayefahamika kama Mashauri Kafura, kwamba aende kwenye ulinzi shirikishi, na kufanikiwa kuondoka nae hadi usiku wa saa nane alipowakabidhi kwa polisi akiwa na wenzake saba.

Akizungumza na EATV, Mama wa marehemu, Pendo William, amesema kuwa mwanaye alichukulia kwa ajili ya ulinzi shirikishi na kupelekwa moja kwa moja kwenye kituo cha polisi Magu, lakini baadaye alipatikana na kesi ya kuvunja koki ya bomba la maji.

"Wamekaa pale kituo cha polisi Magu ndiyo mwanangu akakutwa na kesi ya kuvunja koki ya bomba la maji , kuna askari mmoja wa kike baada ya kufika pale akaanza kumgombeza na kumwitia maaskari wanne wa kiume wakaanza kumsulubu na kumvunja miguu na sikio lake kuchomwa na baadaye tukapata taarifa kwamba amefariki", ameeleza Mama mzazi wa marehemu.

Saidi Haruna ni baba mzazi wa Masudi Saidi, anayedaiwa kufariki akiwa mkononi mwa polisi, amesema wamegoma kuuzika mwili wa mwanae hadi hapo waliosababisha kifo hicho watakapochukuliwa hatua za kisheria.

"Huwezi ukachukua mtu alikuwa mzima halafu ukamzika na majeraha, mimi siwezi kuzika mpaka nielewe huyu aliumia vipi", amesimulia Baba mzazi

Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Gideon Msuya, akizungumza na EATV amesema kuwa hana taarifa ya tukio hilo na kuahidi kulifuatilia.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya