Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali yaagiza kuanza ujenzi madarasa nchi nzima

Sunday , 24th Jan , 2021

Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) David Silinde ameagiza Halmashauri zote nchini kuhakikisha hakuna mwanafunzi anayekaa chini kwa kukosa madawati au kusoma chini ya miti kwa upungufu wa madarasa na kuagiza ujenzi wa madarasa-

Picha ikiwaonesha wanafunzi kutoka moja ya shule nchini (picha na mtandao) kulia ni Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) David Silinde.

katika wilaya zote uanze mara moja kwa yale maeneo yenye upungufu wa madarasa.

Silinde ametoa maagizo hayo alipotembelea shule ya msingi King'ongo iliyopo wilaya ya Ubungo mkoa wa Dar es Salaam kufatia agizo la Rais Dkt. John Magufuli la kutaka ujenzi wa madarasa ya shule hiyo ukamilike kwa haraka, baada ya kuona video ya watoto wa shule hiyo wakisoma chini ya mti.

Silinde amesema serikali ilitoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa madarasa maeneo mengi ya nchi katika mradi wa lipa kwa matokeo EP4R tangu mwezi wa Juni, 2020 lakini madarasa bado hayaja kamilika katika baadhi ya maeneo lakini kwa ujenzi wa madarasa katika shule ya King'ongo utakamilika ndani ya wiki zisizozidi tatu na kutaka watendaji katika wilaya zote kukamilisha ujenzi bila kusukumwa na viongozi wa kubwa wa nchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo  Beatrice Dominic amemwambia Naibu Waziri wa TAMISEMI kuwa ujenzi wa madarasa huo utakamilika Januari 31, 2021 na hadi Februari  5, wanafunzi wataanza kuyatumia madarasa hayo na mpaka kukamilika yatatumia zaidi ya shilingi milion 205 yakiwa ni ujenzi wa vyumba tisa vya madarasa ambavyo vitakuwa na madawati yake pamoja ujenzi wa choo chenye matundu 12.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava