Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Samaki waliokufa waibua hofu Ziwa Victoria 

Monday , 1st Mar , 2021

Wakazi wa Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera, wamekumbwa na hofu ya kulishwa samaki wanaookotwa ziwani na wavuvi wakiwa wamekufa, baada ya kuonekana uwepo wa samaki wengi wanaoelea katika ziwa Victoria, ambao chanzo cha kifo chao bado hakijafahamika.

Samaki aina ya Sangara waliokutwa wamekufa ziwani

Wakizungumzia tatizo hilo baadhi ya wakazi hao wamesema kuwa kila mwaka kati ya mwezi Januari na Februari huonekana samaki aina ya sangara waliokufa wakielea ziwani ambao huokotwa na kutumiwa kama kitoweo, lakini wa sasa wameharibika kiasi kwamba hawawezi kuliwa, huku baadhi ya wavuvi wakidai uwepo wa samaki hao ni neema kwao.

Afisa Uvuvi mkoa wa Kagera Ephrazi Mkama, amewataka wananchi kuchukua tahadhari na kutotumia samaki hao kama kitoweo, ili kuepuka kupata madhara endapo watakuwa wamekufa kutokana na kula chakula chenye sumu.

Kwa upande wake Mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania -TAFIRI- kituo cha Nyegezi Mwanza, Enock Mlaponi, amesema kuwa wamekwishachukua sampuli za samaki hao na kuipeleka kwa Mkemia Mkuu ili kuona kama wana madhara kwa binadamu na sasa wanasubiri majibu, huku akidai kuwa inawezekana wanakufa kutokana na kukosa hewa ya oksijeni ya kutosha.

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP