Thursday , 19th Aug , 2021

Kocha wa timu ya taifa ya Tanzania taifa Stars Kim Poulsen ameita kikosi cha wachezaji 28 kitakachoingia kambini Agosti 24, 2021 tayari kwa maandalizi ya michezo miwili ya kuwania kufuzu fainali za kombe la Dunia, dhidi ya timu ya taifa ya Dr Congo na Madagascar.

Kocha Kim Poulsen

Kwenye kikosi hicho kocha Kim amemjumuhisha golikipa wa zamani wa Yanga Metacha Mnata ambaye kwa sasa hana timu ni mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba na klabu ya Yanga, lakini pia kiungo wa Yanga Zawadi Mauya ameitwa kwa mara ya kwanza. Taifa stars itacheza mchezo wa kwanza ugenini Septemba 2, 2021, dhidi ya wenyeji Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo na siku tano baadae Tanzania watakuwa wenyeji wa Madagascar kwenye mchezo utakao chezwa Dar es salaam. Na hii ni michezo ya kundi J.

Hiki hapa kikosi kamili cha Tanzania Taifa Stars