
Basi la Kampuni ya Fikosh lililopata ajali mkoani Kagera
Akizungumzia ajali hiyo Mkuu wa wilaya ya Bukoba Moses Machali, amesema kuwa basi hilo lenye namba za usajili T710 BXB, linafanya safari zake kati ya mkoa wa Kagera na Mwanza na kwamba wakati linapata ajali lilikuwa likitokea mkoa wa Mwanza.
Kamanda wa polisi mkoani Kagera Revocatus Malimi amethibitisha kutokea vifo hivyo na kwamba miongoni wa waliopoteza maisha watatu ni watu wazima na mmoja ni mtoto mdogo.