Thursday , 23rd Sep , 2021

Siku chache baada ya kuachia smash hit yake “Away” aliyompa shavu Young Lunya, Maua Sama amepanga kuachia kolabo yake nyingine tena akiwa na mkongwe T-Pain kutoka Marekani siku ya ijumaa.

Msanii T-Pain na Maua Sama

Maua amerejea akiwa na nguvu mpya baada ya hivi karibuni kutangaza kuwa amepona matatizo yake ya kiafya yaliyokuwa yakimsumbua kwa takribani nusu mwaka na kuwa kimya kimuziki.