Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kinu cha uji wa moto chalipuka na kujeruhi

Saturday , 25th Sep , 2021

Wafanyakazi 40 wa kiwanda cha Nondo cha Nyakato jijini Mwanza, wamejeruhiwa na mlipuko wa moto uliotokea kiwandani hapo jana Septemba 24, 2021, baada ya kinu cha uji wa moto kulipuka ambapo waliokuwa karibu ndiyo walioathiriwa zaidi na joto la uji wa vyuma.

Wafanyakazi wa kiwanda cha Nondo waliolipukiwa na uji wa moto

Majeruhi hao walifikishwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Mwanza Sekou Toure, na kupokelewa na daktari wa magonjwa ya jumla wa hospitali hiyo Dkt. Diana Anatory, ambapo amesema baadhi yao walikuwa wanalalamika kuwa na shida ya upumuaji pamoja na kuwa na majeraha ya mwilini.

Kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Mwanza, Ambwene Mwakibete, alisema mlipuko huo wa joto la uji wa vyuma umewaathiri wafanyakazi waliokuwa eneo hilo na wengine waliokua mbali wameathirika kwa kurukiwa na uji huo na amewataka wamiliki wote wa viwanda kuchukua tahadhari kwa wafanyakazi wao kwa kuhakikisha wanavaa vifaa vya usalama na kujikinga na madhara ya moto.

Aidha kwa mujibu wa taarifa ya daktari majeruhi 33 waliruhusiwa kurudi nyumbani na majeruhi saba walilazwa.

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Makamba

Ziara ya Rais Samia Korea kuanza rasmi Mei 31 2024

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20