Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kariakoo yote kusafishwa, wenye meza kuondolewa

Saturday , 16th Oct , 2021

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, amewataka wote wanaofanya biashara kwenye maeneo yaliyokatazwa kutumia siku tatu zilizosalia kuhama ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla

Hata hivyo RC Makalla amemuelekeza mkuu wa wilaya ya Ilala, kuhakikisha wafanyabiashara wote waliopanga meza katikati ya barabara za mitaa, Kariakoo na Msimbazi kuondolewa ili barabara zibaki wazi kwa ajili ya magari kushusha mizigo.

RC Makalla ametoa maelekezo hayo wakati wa kikao cha kupokea taarifa ya utekelezaji wa maelekezo ya kuwapanga machinga kwa kila wilaya ambapo amesema kwa hizi siku tatu serikali itaongeza nguvu kwenye kutoa matangazo na elimu ili kuhakikisha ifikapo Oktoba 18, 2021, kila mfanyabiashara awe kwenye eneo alilopangiwa.

RC Makalla pia ameelekeza maeneo yote watakayopelekwa wafanyabiashara ikiwemo masoko, daladala zishushe abiria kwenye maeneo hayo ili kuchochea biashara.

Miongoni mwa wafanyabiashara wanaotakiwa kupangwa ni wale waliojenga vibanda juu ya mitaro na mifereji, wanaofanya biashara kwenye maeneo ya watembea kwa miguu, wanaofanya biashara kwenye hifadhi ya barabara, wanaofanya biashara mbele ya maduka, na wanaofanya biashara kwenye taasisi za umma zikiwemo shule.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto

Picha ya AY kulia na Mr II Sugu kushoto

AY Starring wa muziki wa BongoFlava