Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wazawa 7,713 waajiriwa bwawa la Nyerere

Sunday , 17th Oct , 2021

Katika kuendelea kuhakikisha wananchi wanapata ajira za kudumu za zile za muda mfupi ili kujipatia kipato, serikali imeweka wazi kuwa kipaumbele cha ajira katika miradi ya ndani ni kwa wazawa wenye sifa.

Sehemu ya mradi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere

Hayo yameelezwa na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa wakati akitoa taarifa ya wiki, ambapo amesema katika mradi wa ujenzi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere asilimia 89 ya wafanyakazi ni watanzania.

''Mradi wa ujenzi wa Bwawa la Umeme la Julius Nyerere una Wafanyakazi Watanzania 7,713 sawa na 89% ya wafanyakazi wote 8,635. Mpaka sasa Wakandarasi wameshalipwa Sh Trilioni 2.832 kati ya Trilioni 6. 558 zitakazotumika kugharamia ujenzi huu,”amesema Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa.

Kwa upande mwingine amesema serikali inaendelea kuifungua nchi kwa kuhakikisha barabara zote zinapitika na kuwawezesha watu kufanya shughuli zao za kijamii na kiuchumi bila changamoto hata kama wapo vijijini iwe rahisi kufikia huduma maeneo ya mijini.

''Hadi Juni, 2021, TARURA imetumia Sh Trilioni 1. 297 kutengeneza KM 24,979 za barabara, KM 955.35 kwa kiwango cha lami, KM 16,857 kwa kiwango cha changarawe pia wamejenga madaraja 231 na makalvati mapya 1,325. Mwaka huu wa fedha, Serikali imeitengea TARURA Bilioni 934,” ameongeza Gerson Msigwa, Msemaji Mkuu wa Serikali.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja