Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwela aeleza mafanikio siku ya kwanza ya mkutano

Wednesday , 20th Oct , 2021

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA Tanzania Samson Mwela amesema siku ya kwanza ya Kongamano la Tano la Mkutano Mkuu wa Tehama 2021 imekuwa yenye mafanikio makubwa baada ya wawekezaji mbalimbali kukubali kushirikiana na serikali katika kukuza Tehama nchini.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA Tanzania Samson Mwela (kushoto) akifanya mahojiano na Irene Tillya,

Mwela ameyasema hayo jioni ya leo Oktoba 20, 2021, kwenye mahojiano na EATVSaa1 yaliyoruka mojamoja kutokea Ukumbi wa Simba ndani ya Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), ambapo amesema huu ni mwanzo tu mengi zaidi yakuja.

‘’Kikubwa ambacho leo tumefanya ni mkutano na wawekezaji ‘Investors Round Table’ na hili jambo limeonekana #LIVE duniani kote, kiukweli kumekuwa na mafanikio makubwa sana kwasababu wameonesha nia ya kushirikiana na serikali kwenye kukuza Tehama nchini,’’ amesema Samson Mwela, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Tehama.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya TEHAMA Tanzania Samson Mwela (kushoto) akiwa kwenye mkutano.

Aidha Mwela ameongeza kuwa, ‘’Siku ya leo imekuwa na mafanikio sana mwitikio wa watu umekuwa mkubwa sana, tunatarajia kesho watu watazidi kujitokeza zaidi kwasababu tunajadili masuala ya msingi hususani taifa na uchumi wa kidijitali jinsi gani watu watatumia Teknolojia kujiletea maendeleo,’’.

Kuhusu ujenzi wa taifa la kidijitali Mwela ameweka wazi kuwa, ‘’Tunafahamu suala la kodi linaonekana ni changamoto na limeongelewa, sasa jinsi gani taifa linufaike kupitia Tehama kwenye kukusanya kodi na tumekubaliana, jambo la msingi sasa ni kuangalia tu ni namna gani mifumo yetu itatumika,’’.

Washiriki mbalimbali wa mkutano wakiwa kwenye Ukumbi wa Simba ndani ya AICC.

Pia Mwela amedokeza kuhusu mjadala utakaoendelea kesho kwenye mkutano kwa kusema, ‘’Kesho tutaangalia uchumi wa kidijitali, jamii ya kidijitali na utawala wa kidijitali kwahiyo haya yote ni masuala ya msingi leo tumeanza tu ila kesho tutaendelea kwa upana wake,’’.
 

HABARI ZAIDI

Sehemu ya Ardhi iliyoathirika na Mabadiliko ya Tabia Nchi

Hizi hapa sababu za hali ya hewa isiyotarajiwa

Picha za Satelaiti Zikionyesha Mwenendo wa Kimbunga Hidaya

Kimbunga Hidaya chaendelea kutawala eneo la Pwani

Madaktari Bingwa wa Mama Samia Wakiendelea na Upasuaji

Uvimbe wa kilo 5 waondolewa tumboni kwa mwanamke

Rocket Mwashinga, Chifu Mkuu wa Kabila la Wasafwa

Chifu Mwashinga akemea washirikina kutesa watu

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza na Wanahabari na Wadau wengine kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma leo Mei 03, 2024.

Watendaji serikalini ondoeni ukiritimba - Majaliwa

Kamanda wa Polisi mkoa wa Morogoro SACP Alex Mkama, akionesha vitu vilivyokuwa vimeibiwa

Fundi ujenzi mbaroni mauaji ya dada wa kazi

Wahitimu wa Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT

Wahitimu JKT watakiwa kulinda miradi ya serikali