Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Simba SC watamba usiku wa tuzo za TFF

Friday , 22nd Oct , 2021

Mabingwa watetezi wa ligi kuu, klabu ya Simba imefanikiwa kuzoa tuzo nyingi, tuozo 6 kwenye hafla ya utoaji tuzo ambayo ilifanyika usiku wa jana Oktoba 21, 2021 kwenye ukumbi wa Mwl JK Nyerere Jijini Dar es salaam. Yanga iliondoka na tuzo 2 ilhali Azam, Coastal na Mbeya City walipata moja.

Baadhi ya wachezaji wa Simba wakishika tuzo zao baada ya kuibuka washindi.

Tuzo iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ni pamoja na tuzo ya mchezaji bora Ligi kuu ambayo imeenda kwa nahodha wa Simba John Bocco akiwashinda Mukoko Tonombe (Yanga)  na Clatous Chama (Simba).

Utoaji wa tuzo hizo umefanyika mbele ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye usiku huo. Tuzo zote pamoja na vikosi bora vya msimu ni kama zifuatazo:

Mshambuliaji wa Namungo, Reliants Lusajo ametwaa tuzo ya mfungaji bora wa Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC).

Lusajo katika michuano hiyo alifunga mabao manne na tuzo yake imepokelewa na mtendaji mkuu wa Namungo, Omari.Ruvuma Queens imechukua tuzo ya timu yenye nidhamu Ligi Kuu ya Wanawake (SWPL)

Nahodha wa Simba, John Bocco amepata Tuzo ya mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu wa 2020/2021. Katika msimu huo Bocco alifunga jumla ya mabao 16.

Timu ya Coastal Union imeshinda tuzo ya timu yenye nidhamu ikizifunika Mwadui na Simba.

Meneja wa Uwanja wa Nelson Mandela uliopo Sumbawanga, John Zwala ameibuka Meneja Bora wa Uwanja kwa msimu wa 2020/2021.

John amewashinda Sikitu Kitakala (Azam Complex, Dar), na Midestus Mwalukwa (Sokoine, Mbeya).

Kamishina wa mechi, Pili Mlima kutoka Arusha ameshinda tuzo ya tuzo Kamishina bora wa mechi

.Seti bora ya Waamuzi wa msimu uliopita ni ile iliyochezesha mechi kati ya Simba na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa.

Waamuzi hao ni Ahmed Arajiga, Reonard Mkumbo, Hamdani Said na Hellen Mduma.

Sikudhan Mkulungwa, amepata tuzo ya mwamuzi bora msaidizi kwa Ligi Kuu ya Wanawake

. Amina Kyando Mwamuzi Bora Ligi ya Wanawake Tanzania akiwashinda Tatu Malongo na Esther Adabert.

 Frank Komba Mwamuzi bora msaidizi wa Ligi Kuu Bara na amewashinda Ramadhan Kayoko na Emannuel Mwandemwa.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya