Monday , 8th Nov , 2021

Mwanafunzi wa kidato cha pili shule ya sekondari Mizimbini Kibada mkoani Dar es Salaam Awadhi Matondo (17), anatafutwa baada ya kuzama baharini Novemba 6, 2021, eneo la South Beach Kigamboni akiwa na wenzake watano ambapo wenzake wamepatikana mmoja akiwa amefariki.

Awadhi Matondo, kijana anayetafutwa

Taarifa zimeeleza kwamba kati ya wanafunzi hao watano mmoja alijiokoa mwenyewe, watatu waliokolewa na mmoja wao alifariki dunia na wawili hali zao zinaendelea kuimarika lakini Awadhi hadi leo bado hajapatikana.

Hivyo familia ya Awadhi imesema kwa yeyote atakayefanikiwa kumuona ama kuuona mwili wake apige simu kwenda namba 0754318762 au 0787332246.