
(Abdihamid Moalin akiwa na CEO wa Azam FC, Abdulkarim Amin 'Popat')
Moallin ambaye ni Mmarekani mwenye asili ya Somalia, alisaini mkataba mbele ya Afisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Abdulkarim.
Kocha huyo aliyewahi kuifundisha Horseed ya Somalia, pia atakuwa akifanya uchambuzi wa mechi za timu kubwa ya Azam FC.
Pia amewahi kufanya kazi kwenye Ligi Kuu ya Soka Marekani (MLS), katika timu ya Columbus Crew (2014-2016), kama Kocha Msaidizi wa timu hiyo na timu za vijana chini ya miaka 18 na 23 ikiwemo D.C United.